Dili la Msuva Kutua Yanga Baba Yake Afunguka Ukweli
Bao la Kwanza la Yanga dhidi ya KMC Ilikua Faulo
"Ushindi wa jana wa Yanga 70% percent umetokana na makosa ya KMC, na Ubora wa Yanga ni kwa 30% percent"
"KMC walikuwa na poor defending, tazama Aziz Ki alikuwa hakabwi vya kutosha.. Magoli (2) ya kwanza yametokana na mabeki kushindwa kukaba vya kutosha"
"Halafu ile kona iliozaa bao la (1) ilioanzishwa na Aziz Ki ilikuwa faulo kabla haijatokea, lile halikustahili kuwa goli"
©️ Geof Lea
Mchambuzi wa Efm radio
Yanga Vs KMC - Highlights ya Magoli Yote
Dakika 45 za burudani zilimalizika katika dimba la Azam Complex, Chamazi, Wananchi wanaupiga mwingi mpaka unamwagika.
HT: Yanga SC 1-0 KMC FC
⚽ Job 17'
Ni katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania bara.
Dakika 90 zumemalizika Kwa Magoli 5-0
FT: Yanga SC 5 -0 KMC FC
TAZAMA MAGOLI YOTE HAPA
Ratiba Ya Mechi za Leo NBC Premier League - 23/08/2023
Yanga Vs KMC Live
๐ ๐๐ง๐๐๐๐๐ฌ๐ฐ
๐ NBC Premier League
⚽️ Young Africans SC Vs KMC FC
๐ 23.08.2023
๐ Azam Complex, Chamazi
๐ 1:00 Usiku
Kuelekea Mechi Yetu v KMC Kwenye Head To Head Tangu Timu Ya KMC ilipopanda Daraja Na Kucheza Ligi Kuu Tanzania Bara
Wamekutana Mara :10
Yanga Kashinda Mara :7
KMC Kashinda Mara :1
Wametoka Sare Mara :2
Yanga Magoli Kufunga :13
KMC Magoli Kufunga :5
๐️ ⚽ Leo Tazama mpira live kupitia Simu,
Bonyeza Link Hapa | NI BURE
๐๐๐
https://bit.ly/Watch-Tazama-video-Hapa
©Sokalive
Siri Ya Yanga na Bruno Ngomezi Yavuja
BRUNO Gomez, ni mingoni mwa wachezaji ambao wapenzi wa Yanga walitamani kumuona kikosini mwao msimu huu, chanzo changu ndani ya Singida FG, kimefunguka kuwa pamoja na watu wa Yanga kumtamani Bruno, lakini Mbrazil huyo hakubaliki na uongozi wa juu pamoja na makocha wao.
“Kuna viongozi wa juu kabisa Yanga hawamkubali Bruno. Wanasema bado anahitaji muda zaidi wa kukomaa kumudu kucheza Yanga japo wanaukubali uwezo wake. Nadhani hata makocha (wa Yanga), hawamkubali sana ndio maana hukuona nguvu ikiwekwa kumsajili,”
Kocha wa Singida, Hans van der Pluijm alipoulizwa iwapo kiungo huyo ana nafasi katika kikosi cha Yanga, alisema: “Bruno ni mchezaji mzuri, ila bado anahitaji kukua zaidi kuweza kuhimili kucheza Yanga. Kuchezea Yanga au Simba si kitu kidogo, kule unahitaji uwe umekomaa hasa kuweza kukabiliana na presha za mchezo na mashabiki. “Kule Yanga anaweza kukosea mara moja, mara mbili, mara tatu... mashabiki wakamzomea na kumtoa kabisa mchezoni, hivyo anatakiwa kubaki hapa (Singida) ili aendelee kukomaa zaidi.
.
.
.
Klabu ya Yanga imethibitisha kukamilisha usajili wa beki wa kulia Kouassi Attohoula Yao
๐จ OFFICIAL & CONFIRMED:
Klabu ya Yanga imethibitisha kukamilisha usajili wa beki wa kulia Kouassi Attohoula Yao kutoka Asec kwa Mkataba wa mwaka mmoja.
Yao (26) ๐ฎ๐ช anahesabika kuwa beki bora wa kulia pia na ubora wa kucheza kama winga mshambuliaji na kupiga krosi za mabao.
MFAHAMU KOUASSI ATTOHOULA.
Jina kamili: KOUASSI ATTOHOULA YAO.
Watu wa nyumbani kwao wanapenda kumuita kwa jina la KOUASSI ATTOHOULA YAO.
Raia wa Ivory coast
....Alizaliwa Anyama,Ivory coast
mnamo Dec 20,1996 (Age 26)
Ana urefu wa 1.68m.
Wakala :VV Consulting.
⬛ Nafasi anayochezea ni beki wa kulia
.... Nafasi nyingine anayoweza kucheza ni beki wa kushoto/winga.
Alianza maisha ya soka kwenye akademi ya Mimosas na kuitumikia akademi hiyo kwenye vikosi vya U17 na U19.
✅Julai 1,2017 akasajiliwa na klabu ya Williamsville ya nchini humo akitumikia kwa miaka miwili.
✅Akauzwa kwenda klabu ya O.Khouribga ya nchini Morocco Jan 16,2019 aliitumikia kwa miezi 6 kisha akatolewa kwa mkopo kwenda kwenye klabu ya Kawkab Marrak mnamo Julai 17,2019.
✅ Mnamo Sep 15,2019 baada ya mkataba wa mkopo kuisha alirejea kwenye klabu yake ya O.Khouribga.
Na mkataba wake ndani ya klabu hiyo uliisha miezi miwili baade.
✅๐กNdipo akajiunga tena na klabu ya Asec Mimosas ya Wakubwa Nov 9,2020.
MASHINDANO YA CAF KAMA MCHEZAJI
✅ Amecheza jumla ya mechi 35 ya mashindano haya ya CAF ngazi ya vilabu.
...CAFCL
Amecheza mechi 27, kati ya hizo ni mechi 5 tu alitokea benchi.
..... CAFCC
Amecheza mechi 8, kati ya hizo ni mechi 1 tu alitokea benchi.
Akiwa ligi ya Morocco alicheza mechi 9 na kufunga goli 1.
Aug 27 mwaka jana akiwa na umri wa miaka 25,miezi 8 na siku 7 alicheza mchezo wake wa kwanza kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Ivory Coast chini ya kocha Jean Louis Gasset.
Mpaka sasa ameichezea hiyo ya taifa (michuano ya CHAN,na timu ya taifa ya pamoja) michezo 6.
Aliwahi kuwa beki bora wa msimu wa ligi kuu Ivory Coast 2021/22.
Alikuwa miongoni kwa walioiunda kikosi bora cha msimu ligi kuu ya Ivory Coast kwenye msimu wa 2021/22 na msimu uliopita wa 2022/23
Mshindi wa Makombe mawili ya Ligi kuu Ivory Coast
Mshindi wa Makombe mawili ya FA.
Jezi Mpya Za Yanga Msimu Mpya Wa 2023/2024
Kama Ulikua hujaziona jezi mpya za Yanga SC hizi ndio zenyewe.
Mbunifu wa jezi ya Nyeusi ya Yanga SC kwa msimu huu ameeleza maana ya jezi hiyo huku akijikita kwenye Michoro iliyopo, ameeleza kua;
Jezi ya nyeusi, ukiangalia inamichoro ya 88 na michoro hiyo ilivyokaa imekaa katika mafungu manne ambayo yanamadisha medali nne walizopata Klabu ya Yanga SC
Pia Ameeleza kua ndani ya michoro hiyo kuna Nyota, ambazo zinaeleza kizazi cha nyota au dhahabu ambacho ni Yannga SC ambayo imepitia wakati mzuri mzimu huu.
Kwa Chini kuna nyuzi mzunguko na nembo ambayo ina "Y"; huo mzunguko ulijishikiza katika nembo inawakilisha medali Yanga SC ilizopata na Hiyo Y inamanisha Yanga SC
Je, una maoni gani?
Mbunifu wa jezi ya Yanga SC kwa msimu huu ameeleza maana ya jezi ya njano huku akijikita kwenye Michoro iliyopo, ameeleza kua;
Jezi ya njano maana yake inaelezea matokeo mazuri ya kutokufungwa kwa klabu ya yanga mara nyingi na kutwaa ubigwa
Lakini pia ameeleza kuwa, ukiangalia michoro iliyopo ni ya mchezo mahili wa kupanga matofali ili yasoporomoke, mchezo ambo unahitaji akili na na weredi wa hali ya juu.
Hiyo inamanisha mipango mathubuti iliyofanywa na Aliyekua kocha wa Yanga SC Nasreddine Nabi ya kuweka vizuri timu hiyo na kuvunja rekodi ya kutwaa ubingwa kwa msimu uliopita
Hizo ndizo jezi za Yanga Msimu huu wa 2023/2024
Breaking: Ukweli Kuhusu Mayele Na Yanga SC
Fahamu ukweli kuhusu mayele kuondoka Yanga Sc
Mayele mwenye mkataba wa mwaka mmoja na Yanga amegoma kusaini mkataba mpya ambao ungemfanya awe analipwa pesa ndefu kuliko mchezaji yeyote ndani ya timu hiyo huku akidaiwa amepagawa na ofa nono kutoka Esperance ya Tunisia, Zamalek, Pyramids za Misri, timu za ubelgiji na Qatar.
Kikao hicho kilihusisha pia wasimamizi wa mchezaji huyo ambao wanapushi staa huyo akiwashe Arabuni ambako kuna mkwanja mnene na wako tayari kununua mkataba uliosalia Yanga
Bado hawajafikia muafaka wa kusalia au kuondoka ingawa tajiri ahidi dau nono lakini juzi mchana alionekana kwenye sehemu Jijini Dar es Salaam akipiga picha za matangazo ya uzi mpya wa Jangwani ambao umetangazwa jana usiku nchini Malawai.
Mshambuliaji huyo kupiga picha na uzi wa Yanga kwa ajili ya tangazo ni jambo ambalo linaashiria lolote linaweza kutokea.
Credit: Mwanaspoti
Wana Yanga Sc Wapata Ajali Leo
Taarifa Kutoka klabu ya Yanga Inasema,
"Kuna taarifa za Ajali maeneo ya Msata kwa Mashabiki wetu waliokuwa wakisafiri kuja Arusha kutazama mechi ya kesho.
Tunaendelea kufuatilia kwa karibu, tutatoa taarifa rasmi. Kwasasa tunaomba Dua na Sala zenu๐๐ฝ
#TimuYaWananchi..."
Machi Ya Coastal Union ๐ Young Africans SC
๐ก๐๐ซ๐ง ๐ ๐๐ง๐๐๐ฐ
⚽️Coastal Union ๐ Young Africans SC
๐ 20 Agosti 2022
⏱ 10:00 Jioni
๐ Uwanja wa Sheikh Amri Abeid
๐ #LigiKuu
#TimuYaWananchi
#DaimaMbeleNyumaMwiko
Full Time: Yanga Sc Vs Polisi Tanzaniq
Clabu ya Yanga imeifunga timu ya Polisi Tanzania Ambapo Yanga Imeifunga Magoli Mawili Huku Polisi Tanzania Wakifunga Goli moja
Mchezo umefanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid
POLISI TZ 1-2 YANGA
⚽Kipemba 34'
⚽Mayele 42'
⚽Mwamnyeto 85'
Mabingwa watetezi wa Ligi kuu ya NBC Tanzania bara,Yanga wameanza kampeni za kuutetea ubingwa wao kwa ushindi wa 2-1 dhidi ya Polisi Tanzania katika dimba la Sheikh Amri Abeid
YANGA YASAJILI MCHEZAJI KUTOKA BRAZIL
YANGA YASAJILI MCHEZAJI KUTOKA BRAZIL
Klabu ya Yanga imefikia makubaliano na klabu ya Singida Big Stars juu ya kubadilishana wachezaji Mbrazil Dario Federico Da'Silva JR na Jesus Moloko.
Mbrazil huyo atajiunga na Yanga SC huku Moloko akienda upande wa pili
Kila kitu kinaenda sawa mezani huku dili hilo likitarajiwa kukamilika kabla ya dirisha kufungwa Agosti 31.
#KitengeSports
MANARA, "NIMEINGIA KAMA MC WALA SIJIHUSISHI NA MPIRA"
MANARA, "NIMEINGIA KAMA MC WALA SIJIHUSISHI NA MPIRA"
Aliyekuwa Msemaji wa Yanga, Haji Manara amesema ameshiriki kwenye Siku ya Mwananchi kama mshereheshaji (MC) na sio kama mhamasishaji.
Manara amesema hayo baada ya kutambulisha kikosi cha Yanga mwaka 2022/2023 katika Uwanja wa Benjamini Mkapa.
FULL TIME: YANGA SC 0-2 VIPERS FC
FULL TIME: YANGA SC 0-2 VIPERS FC
๐️ Benjamin Mkapa
YANGA SC 0-2 VIPERS FC
⚽ Karisa 1'
⚽ Anukani 65'
Shughuli imemalizika katika dimba la Benjamin Mkapa, Vipers wameharibu siku ya MWANANCHI baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya wenyeji wao Yanga SC.
Magoli ya wageni yamefungwa na Milton Karisa na Bright Anukani.
Moriso Ashtukiwa, Apewa Siku 14
BERNARD Morrison ameanza kazi rasmi Yanga na leo akiingia siku ya nne mazoezini, lakini kocha mmoja fundi wa mazoezi ameshtukia kitu kwa winga huyo Mghana kisha akamtengea siku 14 za kazi nzito.
Kocha aliyemshtukia BM33 ni Helmy Gueldich ambaye ni kocha wa mazoezi ya viungo aliyeangalia ubora wa mshambuliaji huyo kisha akagundua kwamba jamaa hakufuata sawasawa ratiba ya mazoezi waliyomtumia.
Helmy hata hivyo ameliambia Mwanaspoti kwamba Morrison yuko nusu fiti - nusu unga, lakini ndani ya wiki mbili tu atakuwa katika daraja lingine la ubora.
Kocha huyo alisema katika ratiba ya wiki ya kwanza Morrison atakuwa na kazi ngumu ambayo itamsaidia baadaye kurudisha ubora.
“Tulimpatia ratiba mapema kabla ya kujiunga alitakiwa kuifanya kwa ukamilifu lakini nimemuangalia naona hakuifuata sawasawa ila atakuwa sawa,” alisema Helmy ambaye bado anahitajika Chama cha Soka Tunisia.
“Ni mchezaji mzuri (Morrison) sio mbaya kwa hali aliyokuja nayo kitu kibaya angekuwa hajafuata kabisa lakini tuna muda wa kumrudisha katika mstari.”
Juzi Morrison alikimbizwa mazoezini Yanga akizunguka peke yake pembeni kisha akasimama na kulalamika akiongea kwa Kiswahili akisema: “Huyu jamaa anaiua huyu’ kauli ambayo mashabiki waliokuwa wakiangalia mazoezi hayo nje ya uzio walijikuta wakicheka huku wakishangilia.
Helmy ndiye aliyempunguza uzito beki Djuma Shaban kwa kilo tano kutoka 85 na kubaki na 79 hatua ambayo kocha Nasreddine Nabi amechekekelea akidai beki huyo atakuwa bora zaidi msimu ujao.
Wakati Helmy akimfua Morrison, kocha Nabi amefichua anajipanga kufanya kikao maalumu na winga huyo mwenye mbinu za kupangua ukuta.
Nabi alisema anaamini Morrison atakuwa ni mwiba mkali kwa wapinzani msimu ujao, lakini anataka kukaa naye wakiwa wawili tu kumpa mwelekeo wa maisha ndani ya kikosi hicho.
“Sifanyi hivi kwa Morrison peke yake nimeshazungumza na wengine wote ambao wamekuwa wakifika hapa. Ni vizuri akajua maisha yetu hapa na kitu gani tunakitaka kwake na vitu gani hatakiwi kuvifanya hapa,” alisema.
“Kila mmoja anampenda mchezaji mcheshi na hasa Morrison. Huyu ni mchezaji ambaye tumemsajili kwa mahitaji ya timu hasa malengo yetu kwa msimu unaokuja.”
AGEUKA GUMZO
Kama ulikuwa unadhani BM33 kabadilika kwa vituko pole yako, kwani jamaa amegeuka gumzo kwa wachezaji wenzake wakati wa utambulisho na kusababisha Nabi kupigwa butwaa.
Ipo hivi. Wakati wa utambulisho wa wachezaji wapya ilipofika zamu ya Morrison, kocha Nabi alimtaka ajitambulishe ndipo akafanya timu nzima iangue kicheko.
Morrison akiwa uso mkavu alimjibu Nabi; “Jamani... jamani kocha ujitambulishe wewe, mimi ni mwenyeji hapa.” Jambo ambalo lilimfanya Nabi ashindwe uvumilivu na kuangua kicheko.
Wakati kocha Nabi anaendelea kucheka, Morrison aliendelea na utani wake kwa kuwauliza wachezaji aliocheza nao kabla ya kuhamia Simba alikocheza 2020-2022.
“Nyie mliokuwepo eti hamnifahamu jamani...jamani, wewe Fei Toto na wewe hunifahamu.” Jambo lililofanya timu nzima wacheke wakishindwa kuvumilia kuendelea kumsikiliza.
Hata hivyo, ilimlazimu kocha amwambie apunguze utani na ajitambulishe kisha waendelee na mazoezi na akafanya hivyo.
Wachezaji wa timu hiyo ambao hawakutaka kutajwa majina yao, walisema hadi sasa mchezaji anayeongoza kwa ucheshi na vituko huko kambini ni Morrison anayejichanganya na kila anayemuona mbele yake.
Nje na wachezaji waliyopo Yanga sasa hivi, ambao walicheza naye na wapo na timu nyingine waliyasimulia maisha yake awapo kambini.
Beki wa zamani wa timu hiyo, Juma Makapu ambaye kwa sasa kasajiliwa Ihefu FC alisema Morrison ana vituko na anapokuwepo hapawezi kukosekana mizaha.
“Ni asili yake siyo mambo anayojifunza mnaweza mkaaa na kila mtu akawa na mambo yake anatoka anakotoka anaanza mizaha, naamini huko Avic Town watakuwa na kicheko,” alisema.
Kauli yake iliungwa mkono na Adeyum Saleh ambaye kwa sasa anakipiga Geita Gold “Jamaa ni mcheshi anaweza akaibua jambo hadi ukashangaa, naamini waliyopo kambini watakuwa wanacheka sana.”
Yanga Yapata Mamilioni Mengine kutoka CRDB
Kocha wa Yanga Nabi Agombaniwa
TETESI: Klabu ya FAR Rabat ya Morocco inamtaka Kocha Yanga SC Nasreddine Nabi kwa ajili kuchukua mikoba ya Sven Vandenbroeck klabuni hapo.
Miamba hiyo ya Morocco ipo tayari kumlipa kocha huyo raia wa Tunisia mshahara wa dola 40,000 (zaidi ya Tsh milioni 93) kwa mwezi ili kumng’oa kunako klabu ya Yanga.
Source: #KitengeSports
Yanga Yachagua Meneja na Viongozi Wengine Wapya
Raisi wa clabu ya Yanga Eng. Hersi Ally Said Kwa kushirikiana na Kamati ya Utendaji ya Yanga imewateua Saada Kawemba Kuwa Mkurugenzi wa Mashindano na Walter Harson Kuwa Meneja wa Timu.
Tazama Taarifa Kamili
USAJILI: MCHEZAJI WA YANGA ASAINI MKATABA MPAKA 2024
Mlinzi wa klabu ya Yanga SC Djuma Shabani (29) raia wa DR Congo amesaini nyongeza ya mkataba mpya wa kuendelea kuwatumikia Mabingwa hao wa ligi kuu ya NBC Tanzania bara mpaka 2024.























